SIMULIZI YA SGURD SEHEMU YA KWANZA

MWANZO KABISA SIMULIZI HII YA KUSISIMUA TWENDE NASI






SEHEMU YA KWANZA



                                                                                                                                Na Priva ABIUD


walipokuwa maeneo ya tabata mawenzi, wasijue na cha kufanya
wakiwa wamechoka kwa safari yao ya mizunguko, haruna alionekana
kulegea sana kutokana na njaa, akamwomba rafik yake wapumzike angalau kidogo,
mussa alikataa akamsihi waendele mbele huenda Mungu akasikiliza sala zao,
mbele kidogo walikutana na Yoshua waliesoma nae,
walifurahi sana maana siku hiyo walikurupushwa na mgambo wa jiji,
 wakapoteza makopo yao waliyokuwa wakipeleka kuuza kiwandan,
 istoshe walikuwa na njaa kubwa sana
Yoshua alikuwa ameajiriwa kwenye duka moja kubwa
la tajiri moja mkubwa ambaye alikuwa ni naibu waziri hapa nchin
Yoshua akawapa chakula pia wakatafuta mahali pa kupata maji ya kuoga
 maana siku ya tano hawajaonana na maji kutokana mahangaiko yao.
Walimwelezea rafiki yao huyo shida wanazopata
kutokana na kurupushan za jijin,hivyo hawana kibarua
basi rafiki yao aliamua kuwapa kibarua cha kutembeza bidhaa
za pale dukan ili angalau awe anawapa chakula na sehem ya kujihifadhi

SAFARI YA MAISHA YAO
katika kijiji hiki wanatokea vijana wawili wanaopendana sana
kijana wa kwanza anitwa mussa na wa pili haruna
haruna alibahatika kupata elimu mpaka kidato cha sita mussa yeye alikuwa kijana wa mtaani alishindwa kwenda shule kutokana na matatizo ya kifedha,
waliishi kwa furaha sana huku wakisaidiana kwa namna moja ama nyingine.
 waliishi kwa muda mrefu sana kijijin pale kwa bahati mbaya haruna alishindwa kuendelea na elimu ya chuo kikuu baada ya kukosa mkopo wa serikali
aliamua kujiunga na mussa kufanya vibarua pale kijijin
mussa alikuwa akiishi na mama yao tu ,baba yao alikufa akiwa na miaka kumi pekee. Mwaka mmoja baadae mama yao mzazi aliigua kwa muda refu
lakin kutokana na umasikin mama yao alijitahid kufanya kazi ngumu inagawa bado alikuwa mgonjwa. Kutokana na hali ile mama yake alifarik baada ya
kuugua maradhi ya kifua kutokana na kufanya kazi ngumu
wadogo zake mussa wengine waliacha shule na kuanza
kuufanya kazi ya kuuza karanga na pipi
baada ya mussa kuachiwa majukumu ya familia  aliamua kumwachia mdogo wake familia ili aende mjini kuwatafutia wadogo zake chakula na ada ya shule kwa wadogo zake wawili
wa kike waliokuwa bado wanasoma shule ya msingi
familia yao ilikuwa ya watoto watano yeye akiwa wa sita, hakuwa na uchaguzi
hivyo basi ilimbid akimbilie mjin kutafuta maisha
aliongozana na haruna ambaye alitoroka kwao,
wakalekea jijin dar kwa usafiri wa tren, mwisho walifikia dar lakin wasijue pa kuelekea


JIJIN DAR
baada ya Yoshua kuwapa hifadhi hiyo ,basi ilibid warudi kwa marafiki zao
ambao waliwapokea siku ya kwanza kufika dar maeneo ya gongo la mboto
ambako ndiko walifikia kwa mara ya kwanza kabisa.
 Njian walikutana na majirani wakiwa wamejaa maeneo hayo
jamaa mmoja akawavuta pemben kwa ghafla akawaambiwa
 “wenzenu wale wameshikwa na police, na nyie mnatafutwa, wamekamatwa na kesi ya kuuza bangi na wizi, na wanashutumiwa kesi ya ubakaji
mussa na haruni ilibidi wakimbie na kwenda mpaka tabata MAWENZ
walipofika basi walinyamaza bila kumwambia Yoshua
kesho yake wakaanza kibarua chao huku wakijihadhari sana na ule mkasa uliotoKea jana yake. Maisha yaliendelea na kibarua chao kilwapatia mkate
 mussa alikuwa akiikumbuka familia yake kwa kidogo kile familia aliyoicha nyumban,
ndugu zake wengi walianza kushtumu kitendo kile cha mussa
kutelekeza famailia yao kwa kuiacha familia katika mazingira magumu.
aliishi kwa miaka kama miaka 3 bila kurud kwao, lakin kwa kias Fulani aliweza kuwasaidia wadogo zake sana kwa kila alichopata




AKUTANA NA MAURINE
maurine alikuwa mwenye furaha sana kila walipokuwa wakikutana.
Kila jion baada Ya kazi walikuwa wakielekea kwenye mgahawa mmoja karibu
na nyumba aliyokuwa akiishi maurine, maurine aliipenda sana kampan yake,
alitokea kumwamini sana mussa, alimweleza kila kitu kuhusu maisha yake ya nyuma.
maurine alimwambia kuwa yeye anapenda sana kusoma
lakini hawezi kuendelea na masomo tena kutokana na maisha
maurine alimwambia kuwa wazazi wake walikuwa matajiri wakubwa sana
waliishi dar, lakini yeye aliishi morgoro kwa bibi yake. Akamwelza….
“siku moja ndugu yake mdogo baba aliyekuwa anaishi morogoro alikuwa akifunga harusi.
Siku hiyo Baba, mama na wadogo zangu walikuwa wakitokea dar na gari yake kuja morogoro Kwenye harusi ya mdogo wake, mimi nilimwaga bibi Nikaelekea stand kuu moro
 ili kumpokea baba. nilienda stand saa 6 mchana kuwasubiria
 muda mrefu ulipita bila kuwaona baba na mama na wadogo zangu watatu,
nililia sana kwanini baba na mama walinidanganya, niliamua kurudi nyumban.
Niliamua hata nilisusa hata kwenda harusini yay a baba mdogo.
nilipofika nyumban bibi aliniambia labda wamepata dharura nilimkuta bibi anangalia tv,
baada ya dakika kadhaa walikuja watu watatu nyumban, wakamwomba sana bibi
aende hospitali ya mkoa. Tulipofika hospitalin tulimkuta baba mdogo
 amelazwa akiwa na suti yake tulishangaa na kupigwa na butwaa,
hakuna aliyejua kwanin amelazwa watu walikuwa na huzun wegine walikuwa wanalia tu
ghalfa shangaz nae aliletwa akiwa amepoteza fahamu
bibi alishindwa kuvumilia akawa anapiga makelele akitaka kujua kwanini mwanae kitinda mimba amelazwa maana hakuna aliyemwambia baba mdogo kafanyeje.
mkewe alikuwa pemben na shela asijue cha kufanya nilitoka nje kumtafuta baba na mama nikiamin kuwa walikuja hospitalin ndio maana  hawakuja stand,
nilihangaika hospital nzima lakin cha ajabu sikuweza kumwona yoyote
niliwalaum sana wazaz wangu kwanini ndugu yao kalazwa hawajaja
baba alikuwa mlevi sana, niliamin atakuwa amepita bar na asijue kinachoendelea
baada ya muda baba mkubwa alikuja macho yakiwa mekundu,
akawa analazimisha turud nyumban lakini nilikataa katakat,
nilimuuliza baba mkubwa kuwa baba yupo wapi akaniambia baba yupo nyumban,
sikumwaga mtu yoyote niliondoka kwa spidi nusura nigongwe na pikipiki
ili nimuwah baba na mama niwape taarifa nilipofika nyumban sikuwona mtu yoyote
nilipoingia ndani nilikuta tv aliyokuwa anaangalia bibi bado inawaka
wala hakukumbuka kuizima wakati ule alipopea taarif aende hospital,
 lakini kwenye tv ilikuwa inaonesha taarifa ya habari, lakin cha ajabu
nilishangaa kuona taarifa ya kusikitisha sana, nikiwa naendelea kuangalia sikuweza kuamin nilichona, msomaji wa habari alikuwa akisoma taarifa moja ya kusikitisha sana,
ilikuwa ni taarifa hyo iliyohusu familia moja iliyokuwa ikitokea dar kwenda morogoro
imepata ajali baada ya kugongana na semi iliyoshindwa kukata kona na kuivaa gari ndogo na watu kwenye gari hiyo ndogo wamefariki dunia pale pale.
Lakini majina yao hayakuweza kupatikana mara moja kwa sababu
 miili ya marehemu iliharibika n haikuweza kutambulika mara moja.
Nilihisi kama naangalia filamu, sikutaka kuamini kama ni familia yetu,
Nilijkuta napiga mayowe bila kujitambua, nikaona haitoshi
basi nikatoka spidi nyumban kurud tena hospital, nilipofika hospital
 nilikuta bib nae kalazwa, nikajua basi tayari nimebak peke yangu
nilihisi dunia yote imeniangukia. sikuwa na cha kufanya, nililia mpaka nikazirai.

MAISHA YA MUSSA
maisha ya musa yaliendelea huku akifurahia kibarua chake maana kiliweza kumpa kidogo kitu
alikutana na dada mmoja aliyekuwa akiiuza duka ambalo alikuwa akipeleka oda
waliishia kuwa marafiki hasa kutokana na utan wao
kila siku walipokuwa wakikutana basi walitaniana sana
dada huyo alikuwa mzuri sana wa sura, dada huyo alimpenda sana mussa
jion baada ya kaz dada huyo alikuwa akimpitia mussa kuelekea nyumban
siku nyingine walienda kwenye vibanda vya video au hata wakati mwingine
walienda nyumban kwa dada hyo na walipika wakala
wakati wa usiku musaa anarudi kwenye kibanda chake alichopangisha na haruna
mussa alikuwa mcheshi sana ndio maana dada huyo alimpenda sana
mussa alimficha sana kuhusiaana na maisha yake
lakin haruna aliamua siku moja kumweleza yule dada historia yao
haruna alimweleleza namna maisha ya mussa ya zaman yalivyokuwa
dada yule aliumia sana moyo kutokaana na ugumu wa maisha yake mussa
jonhson nae alikuwa alikumsumbua sana dada yule kila siku hasa akienda dukan pale
alikuwa akimnyanysa na mshahara wake, na pia wakati mwingine
baada ya kumweke mshahara wake benki alimwita nyumban ili tu ampe mshahara wake
jonson alikuwa mtoto wa bossi hivyo maurine hakuwa na uhuru,
jonson alimtaka sana huyu mdada kwa nguv zote lakin mdada yule hakumpenda hata kidogo
siku moja jonson alimwona mussa akiwa na maurine
alikasirika sana , na alikerwa  sana na kitendo kile na alitaman sana hata amfukuzishe kazi mussa kwa sababu Yoshua nae aliajiriwa na Jonson. Hivyo Jonson alikuwa na uwezo
wa kumfukuzisha kazi maana kampuni ile ilikuwa mali yao

TUNAENDELEA
mussa alikuwa akipokea sana pesa kwenye mpesa yake na asijue ni nan anaemtumia
lakin kwa kuwa alikuwana na maisha magumu aliamua kutuma pesa zile nyumban
hata wadogo zake walioacha shule walianza kwenda tena shule
alitaman sana kurud nyumban lakin aliona aibu barua zilikuwa zikija kutoka nyumbna kwao
Hatimaye wadogo zake waliamua kuhamia kwa bibi yao
Lakin huku mjini urafiki wa mussa na maurine ulizid sana
na kitendo kile kinaonesha kilizid kumuumiza sana jonson kichwa
na aliamua kumtumia meseji za matus mussa na vitisho kwa maurine lakin maurine hakujali hilo,
siku moja jonson alituma watu kumkamata mussa kwa nguvu
 Na kumchukua kwa nguvu mpaka nje ya mjin, kwa bahati nzuri maurine na haruna waliona tukio lile hivyo taaratibu waliamua kufuata nyuma
na walipofika maeneo hayo, kwa bahat mbaya jonson aliwaona
 kuwatuma wale vijana wawakamate wote wakaletwa eneo walilokuwa
wakati wanaongea hayo haruna alikuwa akirecod sauti kwenye simu yake
kijana mmoja alimshtukia haruna,akamsearch akamkuta na  simu ikiwa inarecord,

jonson kwa hasira alichukua simu ile na kuipasua yote, akawaagiza vijana wale wawakague kila mmoja mfukon mwao, kumbe maurine nae alikuwa akirecord tukio lile kwenye simu yake
jonson akaichukua simu ile alipotaka kuivunja, maurine alimwomba akampigia magoti
akamwambia chukua memory card pasua ila naomba unipe simu yang ina oda za kazin na mambo muhimu ya kazini, kwa kuwa jonson anampenda sana maurine na hizo oda ni za duka lao, alitoa memory akaificha na kumrudishia simu yake, baadae waliwaachia na wakurudi zao nyumban
mussa alitaka kuachana na msichana yule maana alikuwa akimwingiza
kwenye matatizo mengine, maurine alikataa kata kata, haruna alimshauri sana mussa aachane nae


MAURINE AZINDUKA
Baada ya kuzinduka niliwakuta ndugu zangu wengi Wakiwa pemben yangu wakinipa pole
Sikutaka kuamin kilichotokea Nilitaman sana habari ile siyo ya familia yetu
Ilibid watu watangaze kuwa harus ile imeahrishwa, Maana watu walikuwa wakisubiri ukumbn
Inasemekaa kwamba Waliokuwa kanisan walisema kuwa, baada tu ya harusi kufungwa
Waleiekea kwenye hotel moja kwa ajil ya picha
Wengine walisema Kabla ya tukio hilo la harusi inasemekana kwamba
Shangaz alikuwa akiwasilina na kaka yake ambaye ndiye baba yangu,
Shangazi aliona kimya kwa muda mrefu na wakati mwingine meseji zilikuwa haijibiwi
Akaamua kumpgia simu kujua wamefika wapi mbona wamechelewa
Ghafla alipokea mtu mwingine ambaye alijtambulisha kwa jina la traffic james,
 akimweleza kuwa wanaempigia simu hayupo tena dunian na
 wote waliokuwa kwenye gari hiyo wamepata ajali na wamefriki wote
Shangaz alimkimbilia baba mdogo na kumweleza alichoambiwa, baba mdogo alizirai pale pale.
********************************************************************************
ilipofika kesho yake baada ya tukio, mapadre walifika hospitalin
Kumwangalia baba mdogo lakin bado alikuwa hajazinduka
Tulirudi nyumban, watu wakaja nyumban wakawa wanatupa moyo
Baba mkubwa alikuwa akisema millin ya marehe haiwez kuagwa kwa kuwa iliharibika sana
Madaktar wakasema kuwa ni mtu mmoja tu ndiye mwili ulibak \wengine wote walisagwa na gari, sikutaka kuamin maneno ya madaktari
Nilitaka niwaone hivo hvo ila walinizuia kabisa nisiangalie miile ile
 umati mkubwa hasa wale waliokuwana kadi za harusi wote ulikuja kuzika familia yetu
Baba, mama, wadogo zangu watatu, junia aliyekuwa darasa la 3, Erick aliyekuwa darasa la 5 na Helen aliyekuwa form one
Ulikuwa ni mzigo ambao nilishindwa nifanye, Na wakati ule nilikuwa najiandaa na mtihan wangu kidato cha nne Nilichanganyikiwa kabisa
tuliwazika salama lakin baba mdogo hakuzinduka bado, nilifanya mtihan ule kwa tabu sana
Baadae baba mdogo alizinduka lakin alichanganyikiwa kabisa
Mpaka leo baba mdogo ana matatizo ya akili na amekuwa akianguka ghafla mara kwa mara
Matokeo ya form 4 yalitoka cha ajabu mbali na hali nilifaulu




Mama mkubwa ambaye alikuwa mke wa kwanza wa baba
Alikuja na kutaka mali za baba kwa kigezo kwamba alichangia mafanikio yale
Hivyo anapaswa apewe jukumu la kunilea na kunisomesha maana baba mdogo alikuwa mgonjwa
Mama mkubwa Yule alikuwa mwansheria, alipoenda mahakaman alishinda kesi ile hakuna aliyejitetea, alinichukua nikaish dar na Nilishi nae pamoja na mume wake, lakin mama mkubwa alikuwa akintesa sana. Wakati ule nilikuwa kidato cha tano
Nilisoma kwa tabu, alinipelekesha sana, nilivumilia sana lakin nilishindwa
Nikamaamua kuodoka nyumban na kuanza kujitegemea
Nilimwibia zaid ya million 5 nikakimbia nyumban
Polis walinitafuta na aliniweka rumande kwa wiki moja bila kutoa taarifa kwa ndugu zangu wengine morogoro,
Nilipulizwa kuhusu hizo fedha nilikataa kabisa kuwa sikuchukua pesa ile
Baba mkubwa alipopata taarifa alikuja akanitoa rumande
Niliisha kwa baba mkubwa, baadae alinitafutia kazi kwa rafiki yake ambaye ndiye baba yake jonson, baadae baba mkubwa alihamishwa kikazi mbeya
Akaamua kunitafutia chumba cha kuish ambapo ndicho hiki unacho kiona
Niliahamishia maisha yangu hapa, nilichukua ile million 5 nikajisomesha baadhi ya course za sheria, nikfanya mtihan wa kidato cha sita lakin sikupata matokeo mazuri sana,
nikawa najisomesha open university, Hayo ndiyo maisha yang kaka mussa
*********************************
Siku moja jonson alienda dukan alipokuwa anauza mauirine, maurine alikuwa anajisikia homa siku hyo, akapitiwa na usingizi, akaamua kulala kwenye meza hapo dukan,
Jonson akaingia ndan, akakuta simu yaya maurin ipo mezan, Akachukua simu ile akaangalia baadh ya meseji
Mara ikaingia mesesj ya mpesa alipoifungua akakuta kuwa
Maurine kuna namba ametuma mpesa laki moja
Jonson alipoangalia aliyetumiwa akakutana  na jina la Mussa Jango
Jonson akafunga simu ile akarudisha mezani Akaondoka kwa hasira bila kumwamsha maurine
Akamfuata rafiki yake aitwaye festo,akamwelezea kwamba maurine
Anamtumiaga pesa mussa, festo akamshauri arudi tena pale dukan
Akimkuta bado kalala basi achukue pesa iliyopo kwenye droo.
Jonson akafanya hivyo, ikawa kila siku akienda dukan anachukua kiasi chochote cha pesa
Baadae basi jonson alikuja ili afunge mahesabu, ikaonekana hasara kubwa sana
Jonson  akataka kumfukuza kazi, baba yake jonson akapewa taarifa
Jonson akamweleza baba yake kuwa pesa zimepotea, festo akashauri kwamba
Waende voda shop kubwa waangalie kama huyu dada anatumga pesa kisiri
Walipoongalia walikuta anamtumia pessa Mussa Jango
Baba yake jonson akaomba huyo mussa atafutwe mara moja
******************************************


ITAENDELEA, HII NI RASIMU YA KWANZA, KAMA UNA USHAURI, MTAZAMO AU CHOCHOTE NJOO KWENYE 0763370020/ 0713960030 privashayo@gmail.com facebook Priva abiud

No comments

Powered by Blogger.