ROONEY NI KITABU CHA KICHINA WATU HAWAKIELEWI



ROONEY NI KITABU CHA KICHINA WATU HAWAKIELEWI 

Mashabiki wa Man Utd wakati msimu unaanza zlatan alionekana kama shujaa mpya aliyetokea kuokoa kizazi cha historia kilichobakia akilini mwa kila mshabiki wa Man Utd. Baadae kidogo zlatan huyu huyu alianza kutukanwa na kuonekana hafai, kidogo wakahamia kwa Rooney, wakasema kachoka, kidogo faraja ikarudi kwa goli alilofunga Paul Pogba hivi majuzi. Walio weng nadhani hawajajua hasa ni kitu gani kinaisibu Man Utd. Wapo ambao tayari wameshakata tamaa na Jose Mourinho, wengine wanasema mpira wake ni mbovu n.k

 Image result for rooney bicycle kick
****************************************************************************
Binafsi natamani kuona Wayne Rooney akiongezea mkataba wa miaka mingine kama mitano na mshahara mnono. Najua unaweza ukashangaa kwamba rooney huyu huyu ambaye hata kurusha mpira hawezi. Ndio rooney Huyu huyu wanaemnyooshea kidole. Man utd ya sasa sio kama ya zamani, hii ni Man Utd ambayo mchezaji anaelipiwa zaidi ya 170,000 yupo  benchi, man utd ambayo wachezaji wenye thamani zaid ya milion 100 wapo benchi, morgan E32, mikhitaryan E30, Memphis E28 na luke shaw E30. Haikuwahi kutokea katika historia ya Man Utd wachezaji wenye thaman kubwa kias hicho kukaa benchi wakisubiri mchezaji anaelipwa 70,000 kwa wiki Lingaard, na 37,000 rashford wachoke, tena wengine wakisubiri mchezaji wa Bure zlatani atoke ili wao wapate nafasi. 
******************************************************************************
Wakati huo huo Mchezaji aliyeonesha kiwango bora sana msimu uliopita ndugu Martial msimu huu akiwa katika msimu mbovu kabisa kumzidi hata oliver Giroud tunaemdharau kila kukicha. Unapoizungumzia Man Utd huzungumzii, mchezaji wa ghali duniani, huzungumzii mchezaji mwenye maudambwidambwi, huzungumzii, kikosi cha gharama, huzungumzii matumizi makubwa ya fedha, kama huamini nitajie kikosi Ferguson alichobeba nacho ubingwa msimu wake wa mwisho 2012? Katikati alikuwa na Daren fletcher, alikuwepo cleverly Tom, alikuwa hadi na akina Darren Gibson, pembeni butner alikuwa anampokea Evra, kule Evansi, hapa Oshea, mbele walimtegemea welbeck achana na Van Parsie, alikuja hadi bwana mdogo macheda. Yaani ukilinganisha kikosi ch sasa na cha nyuma ni aibu kubwa na fedheha kwa Jose Mourinho. 

Image result for rooney bicycle kickBinafsi yangu kuna shida ambayo naiona ndani ya kiwanja kikubwa cha Old Trafford pamoja na vichwa na mioyo ya wachezaji Man utd. Wanapaswa kwanza waangalie hadhi yao, walinganishe na kikosi cha Ferguson wakati anazifunga Arsenal, Liverpool Man City na Chelsea bora kabisa. Kimeingia kizazi cha akina Leicester City, akina Southampton, kizazi cha Tottenham. Miaka ya nyuma viwanja vigumu vilikuwa Creven Cottage kipindi fulham imejaza akina Etuhu, Conchesky, akina Danny Murphy, kulikuwepo na viwanja kama Upton Park, kuna wanaume walikuwa wanatumwa uwanjani kuchafua tu akina Kevin Davies. Mbali na kuwa palikuwepo viwanja vigumu kwa Fergie kama Goodspark lakin bado Old Trafford palibakia kuwa machinjio
******************************************************************************

Leo hii Old Trafford sio machinjio tena, bali pamegeuka pango la wahuni, United imekuwa na Mastaa wengi waakubwa na wenye viwango vya hali ya juu lakini hadi Burnley nae kajipatia point old Trafford. Asilimia 80 ya wachezaji wa Man utd kwa sasa hawajui nini maana ya wimbo wa GGMU (glory glory Man Utd. Wapo waliokuja kukuza majina (depay) wapo waliokuja kwa sababu waliwekea mishahara mikubwa (shaw, pogba, mikhitaryan} na pia wapo waliokuja kupokea penshen (zlatan na Bastian)
*******************************************************************

Image result for man utd 2012Suala kubwa ni spirit. Wachezaji wa miaka ya nyuma hawakuwa na majina makubwa wala mishahara mikubwa, walikuwa wachezaji wa kawaida, hawakuwa na ufundi huu amabao leo akina Pogba, Mata na Martial wanaounesha. Mara ya mwisho ufundi kuonekana Old Trafford namkumbuka Luis Nan na Dimitir Berbatov tu. Leo kila kitu kipo united ispokuwa spirit, walio na spirit ni kile kizazi cha Fergie tu, angalia akina Valencia, angalia jinsi Rooney anavyopambana, mwangalie Carrick anavyocheza kwa nidham?. Mchezaji wa united anapoteza mpira anasimama utadhan anasubiri kupigwa picha. Ander Herrera ni mchezaji pekee yake ambaye namuona Rooney Ndani yake ambae sio zao za Fergie, sina tatizo na rashford nampa muda. Ukimuangalia Rooney vizuri utagundua ni kitabu cha kichina ambacho wachezaji wenzake hawamwelewi. Ni kama wanamwona haendani na usasa, kama vile hajui kupiga kanzu, hajui kuchopu n.k. lakini wachezaji wa Man Utd wanapaswa wamanwangalie rooney kwa namana anavyopambana na sio namana anavyopeteza mipira. Watu wanacheza kibisho mnoo.. Herrera na Marcos Rojo wanaonekana ni wachezaji pekee ambayo wangepata namba kwenye kikosi kilichotwaa ubingwa wa ligi msimu wa 2012. Sio kwa sababu wanajua chenga au wana maudambwidambwi. La hasha. Ni kwa sababu wanapamabana, Michael Carrick ni kama amepungua lakini hebu mwanagalie yeye na Fellain?
Image result for vidic blood 
Utagundua ile hari ya upamabanaji wa man utd imepungua. Shida kubwa mashabiki wa Man utd wanadhani ni kana kwamba Mourinho hafai sijui anapaki basi n.k sio kweli, fergie alikuwa anacheza soka gani la kutisha? Cha ajabu kwa Fergie ilikuwa nini zaidi ya spirit? Wachezaji wa United wamuige rooney watajua kwa nini katika umri wa miaka 30 rooney hawezi tena kutoa pasi, watu wamesahau taulo la Vidic.    
Image result for vidic bloodHivi unadhani kuna mtu alishawahi kutumia taulo la Vidic? Hakuna.  Taulo lake lilijaa damu kila mara alipokuwa akipamabana na akina Bobby Zamora, kipindi akipambana kumzua daren bent. Walikuwa wakipiga kazi Sio leo akina Uloa na Giroud wanageuka wafalme Old Trafford. Miaka ile Rio Ferdinand alikuwa analala na mabarafu magotini.    
 Akina fletcher walikuwa kama vichaa uwanjan, muulize wenger alikuwa hawapendi akina nani pale united kama sio Carrick na Fletcher, je carrick na fletcher mbali na kuwa hawana ufundi lakini fabregas Rosicky na Nasri walikuwa hawapumui. Achana na hao turudi miaka ya akina Roy kean? Roy kean alikuwa anaachiwa timu na Fergie aongoze zoezi na kumpeleka majina ya kila anayefanya vizuri mazoezin, je leo Mourinho atamwachia nani kama sio rooney?

      Image result for man utd 2012Je rooney ana thaman ndan ya kikosi cha ushindi Old Trafford? Hayupo. Kwanini?  Hawamwelewi ila siku wakimwelewa watapata jibu kwanini mbwa hambwekei mtoto mdogo.

No comments

Powered by Blogger.