NAJUA HATUELEWI KIARABU, XAVI ALITUTUKANA LAKINI ANAWAELEWA WAARABU, TUMPE NAFASI TUMSIKILIZE




NAJUA HATUELEWI KIARABU, XAVI ALITUTUKANA LAKINI ANAWAELEWA WAARABU, TUMPE NAFASI TUMSIKILIZE

Na Priva, ABIUD
“………..huyu bwana mdogo kimuonekano ana manywele kama ya fellain kwa mbali, anapenda kutumia mguu wa kushoto, ana uwezo mkubwa wa kupiga mipira ya (curve) wabongo tunaitwa ndizi, anajua kutengeneza sana magoli kwa utaalamu wake wa kupiga pasi za kukata na kuchopu na pasi ya kupitilizisha katikati ya mabeki au mipira ya kuzungusha. Kwa mfano mwaka 2013 aliweka rekodi ya kutengeneza magoli 23 kwenye michuano yote ikiwa ni pamoja na kutengeneza magoli 17 kwenye ligi kuu Saudia, pia alitajwa kuwa mtengenzaji magoli bora kwa mismu miwili mfululizo 2013 na 2014……….”
“……….Huwa najiuza sana, sisi waafrika tupo busy na nini? Kwasababu mchezaji chipukizi kwetu ni Yule mwenye miaka 25. Waraabu inajulikana wazi kuwa wapo bize na mambo mengi, wachimbe mafuta, wauze, starehe na mengineyo, sisi kazi yetu kubwa ni kilimo tu sasa tunakosa vipi muda wakuwainua vijana wadogo tunasubiri mpaka tuje tuwaone umiseta? Kwanini tusiwachukue wakiwa UMITASHUMTA?...........”
*********************************************************************
 Related image

Unapoangalia maisha ya Lionel Messi nyuma yake palikuwa na kikundi kikubwa cha watu. Messi hajafanikiwa tu kwa juhudi zake binafsi, ingawa Ronaldinho aliwahi kutamka kuwa, hajawahi kumfundisha lionel messi kitu chochote ila lionel messi alijifunza mwenyewe baadhi ya vitu kutoka kwa watu mbalimbali na yeye akiwepo. Nyuma ya messi palikuwepo na Bwana Rondell aliyekuwa mwalimu wa la Masia kuanzia miaka ya 1990s mpaka 2000, wakati messi anijiunga pale akiwa na miaka 13, pia alikuwepo mtu ayeitwa Juan Laporta ambaye ndiye alikuwa raisi wa Barcelona kwa wakati ule ambaye alionekana kuipenda zaid la masia kuliko kununua wachezaji kutoka nje, kama vile Pique, Iniesta, fabregas, xavi na Messi.
**************************************************************

Image result for OMAR ABDULRAHMAN 2000Kule Riyadh Saud Arabia mwaka 1999 kuna mtu anaitwa Abdulrahman Eissa, huyu wakati waarabu wenzie wakichimba mafuta na kwenda maduka makubwa kuulizia Buggat Veyron 4, na Range Rover sport, yeye alikuwa akipitapita kwenye mitaa ya familia za kati, siku moja alipita kwenye viunga vya familia ya Hadhrami ambayo ni jamii ya hadhramaut huko huko saud Arabia na alikutana na kijana Mmoja anaeitwa Omar Abdulrahman (Ommy) ambaye ni kaka yake na akina ahmad, khaled na Mohamed.  Bwana Eissa alimchukua dogo Ommy na kumpeleka klabu ya El Malaz karibu na uwanja wa mtoto wa mfalme Faisal Bin Fahd ambapo mtoto wa mfalme alishangaa sana kipaji cha mtoto huyo na kuuliza kuwa ancheza klabu gani? Baadae alipata nafasi ya kuijunga na klabu ya Al hilal. Ingawa hakuwa na utaifa kamili wa Saud Arab, yeye peke yake alipewa uraia wa nchi hiyo na familia yake kutoswa kupewa uraia lakini baba yake mzazi mzee abdul alikataa katakata akidai kuwa ni ubaguzi wa wazi na uonezi dhidi ya familia yake. Hapa katikati wakati wa mzozo wa uraia kuna mtu mwingine alikuja akaongezeka katika harakati za kumsaidia Ommy, nae anaitwa Al Garoon, ambaye ni rafiki wa Eisa nae alipigiwa simu na Jamaa mmoja aliyekuwa akisaka vipaji vya soka, nae anaitwa Nasser Bin Thaloub ambaye alitokea klabu ya al Ain, bwana esia alimpa habari kuhusu Ommy kuwa ni kijana mzuri na mwenye uwezo wa kipekee. Hapo ilikuwa mnamo mwaka 2000 na Kipindi hiki Messi alikuwa na Umri wa miaka 13, lakini kaka Ommy alikuwa na Miaka 9 tu.
************************************************************************


Image result for african local football streetHuwa najiuza sana, sisi waafrika tupo busy na nini? Kwasababu mchezaji chipukizi kwetu ni Yule mwenye miaka 25. Waraabu inajulikana wazi kuwa wapo bize na mambo mengi, wachimbe mafuta, wauze, starehe na mengineyo, sisi kazi yetu kubwa ni kilimo tu sasa tunakosa vipi muda wakuwainua vijana wadogo tunasubiri mpaka tuje tuwaone umiseta? Kwanini tusiwachukue wakiwa UMITASHUMTA? Yaani unangoja mpaka anafikia TUSA (michuano ya Vyuo Vikuu) ndo mnaanza kusema Yule kijana anakipaji. Kwenye Maisha ya Ommy hapo tumekwisha ona zaid ya watu watatu wanajaribu kuinua kipaji chake akiwa na miaka 9 tu. Mtoto wa kitanzania akiwa na miaka mitano wazazi wanamnunulia mpira mlaini, akifikisha miaka 7 akionekana anacheza mpira, huo mpira unatupwa mabatini au kuchomwa na wazazi wake wazazi hapa wanasahau kama waliwahi kuwanunulia mpira, akiwa na miaka 11 kuendelea akionekana anacheza mpira mzazi atamwita tu makusudi ampe kazi nyingine ilimradi tu asicheze mpira. Huyu huyu kijana mwenye dhamira ya kweli na soka akifikisha miaka 18 bado anakomaa na mpira wazazi wataanza kumlaumu kumpa maonyo kuwa asichezee  elimu, yaani lawama kibao kuhakikisha tu anasoma na sivinginevyo. Basi asipofaulu elimu zaid ya hapo akicheza mpira wa mitaani ataonekana mvivu, mhuni n.k. huyu huyu kijana mpaka aje afikie malengo yake ni miaka 25, hapo ndipo figisu inaanza, anabadili mwaka wa kuzaliwa ilia apate nafasi ya kushiriki michuano ya madaraja ya chini, cocacola n.k ndiposa apate nafasi ya kujiunga samba na yanga.
******************************************************************************

Image result for OMAR ABDULRAHMANWakati Rijkaard anaongezeka kwenye listi ya watu waliomsaidia Lionel Messi anaamua kumpa nafasi baada ya kushauriwa na mwalimu wake bwana Rondell, upande wa pili kule Uarabuni nako tunaona mtu wa tano akiongezeka kwenye listi ya watu wanaomsaidia Ommy kufikia mafanikio yake, nae ni kocha Winfred Schafer alipoamua kumpa ommy nafasi ya kucheza kikosi cha kwanza akiwa na miaka 16 tu. Messi huyu wa Asia alifunga magoli 6 kwenye michezo 10 na kutengeneza mengine matatu. Kwenye mchezo wake wa kwanza kwenye mechi za wakubwa alitengeneza goli pekee tena aliingia uwanjan mnamo dakika ya 77 tu na kutengeneza goli hilo la pekee baada ya kupiga shuti liliogonga mtambaa wa panya kabla ya Dias kuwapa Al ain ushindi. Msimu wa 2009 aliweka kimyani magoli matano kwenye michezo saba, msimu wa 2010 alifunga magoli 11 kwenye michezo 29 na kutengeneza magoli 8 ikiwa ni msimu wake wa pili.
****************************************************************************

Baadae klabu ya Man city walimchukua kwa majaribio, mtu wa 6 aliyeongezeka hapa ni mwalimu wa kikosi cha watoto Man city bwana Brian Marwood aliyemfuata ommy mpaka falme za kiarabu. Alipomkuta aliiomba klabu ya Al ain kumruhusu waondoke nae kwa majaribio ya wiki mbili kwa makubaliano ya kumsajili kabla ya dirisha kufungwa. Alifanya majaribio ambapo klabu ya Man city ilikubali kumpa mkataba. Lakini shida ya vibali ya kazi pamoja na viwango vya FIFA vya taifa lake havikukidhi kwa yeye kucheza ligi kuu England.
********************************************************************
 Image result for OMAR ABDULRAHMAN



Kwanini wanamwita messi, huyu bwana mdogo kimuonekano ana manywele kama ya fellain kwa mbali, anapenda kutumia mguu wa kushoto, ana uwezo mkubwa wa kupiga mipira ya (curve) wabongo tunaitwa ndizi, anajua kutengeneza sana magoli kwa utaalamu wake wa kupiga pasi za kukata na kuchopu na pasi ya kupitilizisha katikati ya mabeki au mipira ya kuzungusha. Kwa mfano mwaka 2013 aliweka rekodi ya kutengeneza magoli 23 kwenye michuano yote ikiwa ni pamoja na kutengeneza magoli 17 kwenye ligi kuu Saudia, pia alitajwa kuwa mtengenzaji magoli bora kwa misimu miwili mfululizo 2013 na 2014. Anacheza kama kiungo wa pembeni anaetokea kushoto, pia anaweza kucheza kama kiungo wa kati mshambuliaji. Ana uwezo mkubwa wa chenga, mwepesi, anakasi, na mmoja wa wachezaji bora kutoka Asia kwa sasa. Tayari umri wake umeenda kidogo sawa, akiwa na miaka 25 tayari ana mafanikio makubwa ndani ya bara la Asia, lakini bado kwa aina yake ya uchezaji binafsi bado namwona ni mchezaji bora ndani ya bara la Asia kwa wazawa.  Tayari ameisaidia klabu ya Al Ain kubebwa ubingwa wa ligi za kiarabu, ubingwa wa ligi, super cup, kombe la Rais, na ubingwa wa AFC. Ametajwa kama mchezaji bora wa klabu mwaka 2008, na 2009, alitajwa pia kuwa mchezaji bora chipukizi 2009, 2010, mchezaji bora wa mwaka kupitia Al Ahram 2010, mchezaji wa thamani kwenye michuano ya ubingwa wa ligi za kiarabu mwaka 2010, mchezaji bora wa mashabiki kupitia AGL 2012, pia aliwahi kuwa mchezaji bora chipukizi kupitia Al Hadath 2013, na mchezaji bora wa Emirate 2013. Mchezaji bora wa bara ya Asia 2016, mchezaji bora wa ABA ligi kuu zote za Asia 2015,mchezaj bora kupitia GSA, AFC 2016, al haram mchezaji bora 2015/6 mchezaji bora wa Emirate kupitia AGL kwa msimu wa 2014/15/16. Yaani ukiangalia vizuri hizi tuzo anatosha kabisa kuwa mchezaji bora wa kiarabu kwa miaka ya hivi karibuni. 

Image result for OMAR ABDULRAHMANHuyu ndiye Messi wa Asia na ndiye mshindi wa Mars D Or mchezaji bora wa kiarabu mwaka 2015. Ukitaka kumjua tu wala usijipe tabu nenda youtube andika tu Omary Abdulrahman utamwona na naamini utaamini yale niliyosema kwa Gabriel Jesus miaka miwilli iliyopita hakika huyu nae akipata nafasi nyingine ndani ya ligi kuu Hispania kati ya Barcelona au Madrid, au hata England ndani ya klabu kama Arsenal Na Liverpool ambazo naona zinanendana na mfumo wake basi nae atamulikwa kama wanavyomuikwa wengine. 

*****************************************************************************

Image result for OMAR ABDULRAHMANMakumpuni kama AGL. AGC, AFC, al harham, al hadaath, OSN, zimembeba sana kijana huyu kufikia hapo alipofika, lengo la makampuni haya ni kutanagaza lulu ambayo waarabu wanajivunia. Je sisi Tanzania ni makampuni mangapi yametoa nafasi kuwatangaza wachezaji wetu kushinda tuzo mbalimbali ili kuwapa moyo wale wadogo kufikia malengo? Kwa ufupi tu huyu ndo Ommy wa kiarabu ambaye yeye ameona hakuna umuhim wa kutojiunga na ISIS na kuamua kufurahisha watu kwenye tv. Lakini binafsi naona Xavi amekuwa kama anatoa kashfa kwa Ronaldo kila kukicha, lakini mnamo mwaka 2015 alimsifia bwana mdogo Ommy na kusema anastahili kuja ulaya. Ni wazi kuwa aliona kipaji chake.


Image result for OMAR ABDULRAHMAN a kid Neymar, luiz david, pamoja na zidane walimsifia sana kijana huyu. Naweza pia kusema tunaweza kumweka kundi la akina Adnad Al Taylani, na akina Ismail Matar. Xavi anasema hajawahi ona lulu kama ile, xavi amekuwa akiimba sana kuhusu huyu mtu, lakini naona ni wakati wa xavi kusikilizwa na yeye, juzijuzi nilibahatika kumsikia Leandro mshambualiaji kibrazili anayekipiga Hyundai ya china, alisema, sijawahi kuona mwarabu kama huyu, ni zaidi ya jini, huenda wazungu hawawaelewi watangazaji wa kiarabu, laiti wangekuwa wanawaelewa wanavyomtangaza  kumpamban ommy anapokuwa na mpira leo hii asingekuwa uarabauni. Xavi amekaa uarabuni, hajui iarabu lakini anayoyaona huko yana umuhimu mkubwa kwa soka la kiarabu hasa kwa ommy mwenyewe



No comments

Powered by Blogger.