ASIPOMWELEWA MARTIAL BASI MKUMBUSHENI YALIYOMKUTA LUIS NANI



 Priva ABIUD.

kijiweni kwetu.

Hivi majuzi nimemsikia David Trazeguet akimsihi sana Kylian Mbappe kuhusu uhamisho wake wa wapi pakwenda. Man Utd imeonekana kutaka kumchukua kinda huyu wa Monaco aliyeanzia Maisha pale yake pale AS Bondy ambako baba yake mzee Wilfred alikuwa kocha. Huyu kijana alizaliwa mwaka 1998, lakini miaka 7 nyuma yake alizaliwa Antonio Griezmann. Wakati luis Nan akijiunga Man Utd mwaka 2007 Mbappe alikuwa na 10 tu. Mbappe na Griezmann wamezaliwa katika maisha mazuri ya kisoka maana wazazi wao wote walikuwa makocha na walikuwa watu ambao walikuwa na uwezo wa kulisha familia yao. Wakati Griezmann, Mbappe na Anthony Martial wakiwa na mazingira mazuri kimaisha hii ilikuwa tofauti na Luis Nani. 
 Image result for santa filomena youth footballer street
Kwa kifupi kuna vitu vingi hawa vijana wanapaswa kujifunza kwa luis Nani kwanza kabla ya wao kufanya maamuzi magumu katika hatma yao ya kesho. Nmetangulia kumzungumzia David Trazeguet, naamini wengi tunamkumbuka David hasa kwenye kombe la dunia la mwaka 2006 pale alipokosa penati ya mwisho na Italia kutwaa kombe la dunia. David anasema kuwa mbappe kwanza ni mdogo sana, hajafikia kiwango cha kuuzwa million 70. Amesema biashara hizi huenda zikaharibu kiwango chake na kikapoteza maisha yake kwa ujumla. Amemsihi sana kutokujiunga Man utd kwa sasa hata kidogo. trazeguet anadai kuwa, mbappe bado hana misuli ya kwenda kubeba mawe pale Old trafford, trazeguet anaamini Old trafford ni shamba ambalo ni gumu kwa Mbappe kuvuna kirahisi ikiwa ndo kwanza maisha yake yanaanza. Mbappe ameanzia maisha yake Monaco akiwa na miaka 16  na siku 347 tu alicheza mechi ya wakubwa akitokea benchi.
Image result for santa filomena youth footballer street

Wakati magazeti yakimtangaza Mbappe na Martial wakiwa na miaka 15 tu, luis Nani katika umri huo yeye alikuwa akipigana na Umasikini na maradhi. tumekuwa tunahisi kuwa kila mtu anayeishi ulaya basi wanatoka maisha mazuri. lakini amini usiamini kuna watu wanatoka maisha magumu ambayo wanakosa hata maji ya kunywa. kwenye umri wa miaka 18 Luis nani alikuwa akipokea kitita cha dola 10000 kwa mwezi. ukitazama kiwango hicho ni kidogo sana kwa Mbappe kwa sasa. kwa umri wa mbappe anahitajika kwa kiasi kikubwa cha hela kama million 70 maana yake mshahara wake hautakuwa chini ya dola laki 2 kwa wiki. ni tofauti sana ukifananisha na mshahara wa Luis Nani akiwa Lisbon.
Image result for santa filomena povertyKatika kijiji cha Santa Filomena kuliko Lisbon huko ndiko alikokulia luis Nani. Katika mitaa ile kijana yoyote aliyekuwa na umri wa miaka 15 alikuwa chokoraa au mwizi. Vijana wengi wa maneno yale walikuwa na hati ya uhalifu wakiatafutwa na polisi kwa makosa mbalimbali ya uhalifu. Nyumba ya akina luis Nani alikuwa na mlango wenye viraka na matundu mengi huku baadhi ya maeneo ya nyumba yakifunikwa kwa Nyasi. 

Katika umri huo wa Luis Nani, mdogo wake Kylian Mbappe tayari Monaco washaanza kumnyemelea na magazeti kibao yalishaanza kumpamba kwenye kurasa za mwanzo tu.

Tricky feet: In action for Sporting in 2007
Baada ya Loius Nan kuhamia santa filomena akitokea Cape Verde, shirika moja lililokuwa likisaidia watoto waliokuwa wakiishi mazingira magumu walimchukua na kumpeleka shrikan kwao. Bwana Alcides Mendes ndiye mtu wa kwanza kuona kipaji cha kijana huyu. Alimchukua Louis Nani na kumpeleka shirikian hapo ili kumkwepusha na makundi ya kiuhalifu yalikuwa yamekithiri mtaani kwao. Louis Nani anasema mara ya mwisho baba yake mzee Domingos alirudi nyumban wakati wa sikukuu akiwa na miaka saba na hakuwahi kurudi tena. Anaongeza pia mama yake Mama Maria do Ceu alikimbilia nchini uholanzi luis akiwa na miaka 12. Maana yake luis nani aliishi kwa kipindi kirefu bila wazazi. Louis Nani anakwambia nyumbani kwao walikuwa watoto 10, hivyo hakuweza kukimbia familia baada ya wazazi wake kukimbia hivyo alibidi abaki santa Filomena kwa shangazi yao huku akisema kuwa chumba kimoja walilala watoto 6. Akiwa mdogo anakwambia kuwa alikuwa anadandia treni kwa nyuma ambayo ilikuwa inakwenda kwa umbali wa maili 6 ambako ndipo alipokuwa akifanya mazoezi ya mpira katika klabu ya Real Massama. katika klabu ya Massana anasema mara nyingi alichezea klabu ile kwa sababu alikuwa akipata chakula na baadhi ya mahitaji yake madogo madogo

United hero: Nani bagged the winner over rivals City in the Community ShieldMendes anasema katika kipindi chote hicho akiwa na kijana Yule, alisema kuwa ni mmoja kati ya vijana waliokuwa hawakati tamaa.  Anasema kuwa wakati Fulani alikuwa akipenda kucheza kwenye timu yenye wachezaji dhaifu ili kila saa awe na mpira yeye na hata wakati mwingine ili ajipe majukumu makubwa zaidi uwanjani.  Mendes anaongeza kuwa ilikuwa ngumu sana kwa kijana kutoka kijiji kile na kwenda duniani akimaanisha ni ngumu sana kwa kijana mdogo katika mazingira yale kufanikiwa kwa kiwango alichofanikiwa Luis Nani.  Anasema alipigania maisha yake pale ureno kwa sababu alikuwa Muafrika na alikuwa akibaguliwa sana mpaka pale alipofikisha miaka 18 alipopata uraia wa Ureno.  Mbali na soka Luis Nan alikuwa nakwenda na kaka yake kwenye shughuli za ujenzi ili kujipatia kitu kidogo cha kula na kulisha wadogo zao. tukiachana kidogo na Luis Nani, Mimi binafsi sina tatizo na Kylian Mbappe kwenda Man utd. Mimi pia naamini ndoto za mbappe ni kucheza klabu kubwa duniani kama Man Utd. Shida kubwa iliyopo katika timu kubwa kama hizo unaposajiliwa kwenye ile klabu ukibweteka kidogo unapotezwa. Klabu kubwa haziangalii maisha uliyotokea, haziangalii historia yako zinaangalia jitihada zako. Luis Nani hakwenda United kwa sababu alionewa huruma, ila alikwenda pale kwa sababu alionesha jitihada kubwa. anthony martail amekuwa na maisha magumu Old trafford. maisha magumu yalimfanya Luis Nani kujiamini na kujipa moyo kuwa ipo siku atakwenda duniani. aliamin kuwa ugumu wa maisha ungempeleka dunia. mbali na hapo bado alaimini kuwa Old Trafford itakuwa shamba lake na atapata yale alikuwa akihitaji wakati akiwa sanata filomena.
Image result for luis nani and mbappe
kwa Upande fulan ni kama vile Martial hajapata somo kutoka  kwa Luis Nani kuwa na kiwango bora kabisa alipobweteka hakuna aliyemgeukia. martial amekuwa si na msimu mbaya tu pia amekuwa na migogoro ya chini kwa chini kama ule wa Luis Nani na Kocha wake mkuu bwana Alex ferguson. ila kwa mbali nmeanza kuielewa kauli ya Trazeguet, ni kama anamwambia Mbappe kuwa Martial ameonja kikombe alichoacha Nani. Mbappe huenda Martial nae akatoa somo kwake, na kama hatolielewa somo hili mapema basi atalielewa akiwa anaondoka Old trafford kama Depay. Umri wa mbappe ni mdogo sana kwa kiwango kile cha pesa, hastahili hata nusu ya pesa zile kwa umri wake. Old trafford ni uwanja wa vita, ni uwanja ambao ulimzawadia Nemanja Vidic mataulo mengi ya kufutia damu ilimradi tu kabati la timu likose vikombe. Vijana wengi hawajui Historia ya klabu ile hivyo wanaendeshwa na hisia za kwamba ipo siku watajengewa sanamu. kufanya waliyofanya akina Japp stam na akina Bobby Robbson huwezi ukawa unashinda saluni hata siku moja. Mbappe kama ataenda Man utd ajue fika kuwa anakwenda kwenye vita wala hakuna majaribio pale. ni uwanja ambao kila wikiendi unajaza wambea zaid ya 70,000 waliobeba mabango yenye historia za babu zake na baba zake wakiimbia GGMU. tuachane na Mbappe tuendelee na Luis Nani....
Head over heels: Nani shows off his 'flip-flop' goal celebrationAnsema staili yake ya kushangilia kwa sarakasi alijifunzia kwa wabrazili Fulani waliokuwa wakija shirikani wakijulikana kama kundi Capoera. Loius nan anasema akiwa anashangilia vile huwa anakumbuka sana maisha aliyotokea na anapenda kumkubuka dada yake wa kike aliyekuwa akiipenda sana staili ile na aliyempa jina la utani. Maisha yake yalikuwa ya furaha sana licha ya kuwa na njaa na umasikini uliokithiri mno. Anakumbuka kuwa katika kipindi kile kazi yake nyingine kubwa ilikuwa wizi wa matunda katika mashamba ya watu. Alikuwa akienda kwenye matukio mabaya na magumu lakini aliukuwa akipata matokeo mazuri kwa familia yake. Anaongeza kuwa kaka yake anayeitwa Paulo ndiye aliyekuwa nguzo muhimu katika maisha yake.  Anaongeza kuwa kuna matukio mabaya yaliyomfanya baba yake asirudi nyumbani. Anasema kuwa mwaka 2006 alikutana na baba yake, kisha baba yake alimweleza kuwa kwanini alikimbia Ureno. Wakati baba yake akimweleza hayo, Luis Nani uchungu ulimpata na akamsihi baba yake kuwa hahitaji baba yake amuombe yeye msamaha kwa kuwa yeye ni mtoto wake na alimweleza kuwa hana tatizo naye. Alikuwa na furaha kubwa kukutana na baba yake. Ni wanaume wachache waliofanikiwa kwenye  maisha wenye moyo kama Luis Nan hasa kwa kitendo cha baba yake kuitenga faimilia. Lakini yeye alimwelewa na alichukulia ni sehemu ya maisha na ni changanmoto tu za kawaida. Mbappe na martial wanapaswa kujifunza kuhusiana na ugumu wa maisha ya Nani katika kuhakikisha kuwa wanafika mbali. Wao wamelelewa maisha mazuri yasiyo na vikwazo na ikiwa walipata bahati ya kucheza klabu kubwa mapema kabisa. wana nafasi kubwa ya kufanya makubwa, wanapaswa waone Old Trafford ni kama  Santa Filomena. wanapaswa watafute mafanikio sio kwa kupenda pesa na sifa bali kwa kuweka jitihada nyingi na kwa kujiamini, kujituma na unyenyekevu mkubwa.
Wakati magazeti leo hii yanamtangaza Mbappe kuwa ndiye Thiery Henry Mpya miaka yake luis Nan alikuwa akipambana na wahuni mitaani. kwa mtazamo wa haraka haraka utagundua utofauti wa maisha ya Santa Filomena na kijiji cha Macon alichozaliwa Griezmann. kwanza wakati Luis Nani akizaliwa katika adha zote hizo kule Cape Verde, Griezmann yeye alizaliwa Hospitalini tena alizaliwa na meya wa mjini na mama yake alikuwa mfanyakazi wa Hospitali. maisha yao  ni tofauti kabisa. huenda hata Griezman akija Man Utd nae akabweteka, hivyo anapaswa ajifunze ugumu wa maisha ya Old trafford. leo hii mchezaji bora wa Ujeruman Henrik Mikhitaryan anateseka ndani ya ukumbi ule. vwanjan vya Old trafford au Santiago vipo mjini lakini maisha yake ni kama kijiji cha santa Filemona. sio sehemu ya Maonesho na pia sio sehemu ya kujifunza bali ni sehemu za vita.

Maisha ni kwenda mbele na kurudi ulipotoka, Baaada ya mafanikio makubwa luis Nan anarudi kijijin Massama alikoanzia soka na kuwapa nguo pamoja na vyakula mara kwa mara. Anakumbuka fadhila alizopewa wakati wa utoto wake hasa kwa vyakula na nguo ikiwa ni kama fadhila. Luis nani anasema kipindi cha nyuma, hakuwa na uwezo wa kununua nguo za mazoezini hakuwa na uwezo wa kununua nguo nzuri, hivyo marafiki zake walikuwa wakimpa nguo zilizochakaa au nguo ambazo zilikuwa hazitumiki. Wakati fulan marafiki zake walikuwa wakimwita nyumban kwao ili wapumzike nae angalau wakati wa chakula aweze kushiriki nao msosi kibongobongo hii tunaita kudoea msosi kwa jirani.
Talent spotter: With Carlos Queiros (right)Mnamo mwezi wa 5 mwaka 2007, Aurelio Perrera alipokea simu kutoka kwa Carlos Queiroz ambaye alikuwa rafiki mkubwa wa Sir alex Ferguson na kocha msaidizi ndani ya Man utd. Queiroz alipata taarifa kuhusu huyu kijana, hivyo walimbeba David Gill mpaka Lisbon. David Gill alikuwa na wasiwasi kuhusu kijana Yule hasa suala la ada ya uhamisho. Carlos alikuwa Hotelini huko Lisbon, na ni mzee mwenye miaka 64 ambaye kazi yake kubwa ni kuibua viwango vya wachezaji wadogo huko huko Ureno. Huyu Carlos ndiye aliyeibua vipaji vya Cristiano Ronaldo, Luis Figo, Paulo Futre, na Ricardo Quaresma. Carlos alipoulizwa kama huyo kijana {luis Nani} ataweza kwenda Old Trafford alishikwa na kigugumizi maana ilikuwa ni dili la takribani million 25. hapo juu nilisema kuwa kiwango cha pesa ambacho mbappe anahitajika nacho ni kikubwa mno, kiasi kwamba ukijaribu kuangalia kiwango alichonunuliwa nacho luis Nani pia kwa wakati ule ni kikubwa mno. Yapo mengi ya Mbappe kuulizwa kama alivyoulizwa Luis Nani kabla ya kusajiliwa. Nani aliulizwa je utaweza kuhimilia makelele na presha ya Old trafford? jibu lilikuwa ndiyo kwakuwa tayari alishajiamini. Luis Nani alitambua kuwa mlango wa Maisha yake umeonekana hakujalish kama akishapita ataufunga au atauacha wazi. Kuna mawili kwa Mbappe, kumsikiliza Trazeguet au kufumba macho kama Luis Nani kufungua mlango bila kujali atakachokutana nacho huko Duniani. Maisha ya luis nani Man utd hayakuwa maraisi hata kidogo, yalikuwa ni maisha magumu yaliyojawa kelele za kila aina, sio kelele za wahuni, ni kelele za wadau wa soka, mashabiki na waandishi wa habari. Baadae Carlos alimhahakikishia david Gill kuwa ni kijana mzuri na mwenye uchu wa mafanikio.
Image result for luis nani and mbappe Baadae luis Nani alifumba macho na akafungua mlango ambao aliamini ndiyo sehemu ya kuanzia maisha yake.  David Gill alikamilisha dili la kijana huyo mwenye miaka 20. Hapo ndipo safari ya duniani kwa Luis Nani ilipoanzia. tukirudi nyuma kidogo katika Maisha ya luis Nani pale Real Massama, yalikuwa ya tabu sana, anasema moja ya vitu ambayo hawezi kusahau ni kwamba siku moja walialikwa na klabu ya Benfica kwenye mechi ya kirafiki, kabla hawajaingia uwanjan unajua  nini kilichottokea? 
Basi ungana nasi kwenye sehemu ya pili ya makala hii

No comments

Powered by Blogger.