..,,,HIVI UNAFAHAMU KWAMBA KATI YAO YUPO MGANDA ALIYEMTOA KIJASHO MOURINHO..?


Na Priva ABIUD. 

Kijiweni kwetu 

Wakati Man Utd ikiumana na Celta Vigo na Midjytland kuna kijana mmoja mweusi alikuwa amekamata dimba la kati kwa jina anaitwa Pione Sisto. Huyu kijana alionekana kung’aa alipokuwa Midjytlan na hata kwenye mchezo wa hivi majuzi akiwa na Celta Vigo. Huyu ntamuongelea baadae ngoja niwazunguzmie kaka zake kwanza;
*****************************************************************************
Image result for DENMARK BEST FOOTBALL TALENTS
Peter Schmeichel
Wakati nazaliwa mnamo mwaka 1992 kikosi cha bwana Richard Moller Nielsen kiliishangaza dunia, kwa kuichabanga Ujeruman waliokuwa mabingwa wa kombe la dunia kwenye michuano ya Euro. Kichapo kile Denmark ilichokitoa  kilimfanya nguli wan Nchi hiyo Michael Luadrup kustaafu soka. Denmark walikuwa wakiongozwa na mlinda mlango anayeaminika kuwa mlinda mlango bora kuwahi kutokea Bwana Peter Schmeichel. Hicho ndicho kilikuwa kizazi bora kwa Denmark kwa wakati ule na katika Historia ya nchi hiyo. 

Katika historia ya taifa ile hatuwezi kuacha kumzungumzia Brian Laudrup ambaye amewahi kutwaa tuzo ya mchezaji bora wa Denmark kwa mara nne na pia aliwahi kutajwa na FIFA mwaka 1992 kuwa mchezaji wa tano kwa ubora duniani kwa mwaka ule. Ni mchezaji ambaye sima wa soka kutoka Brazil Pele alimtaja katika orodha yake kuwa ni mmoja kati ya wachezaji bora dunian kuwahi kutokea duniani akimweka nafasi ya 125.
Image result for laudrup and his brother michael laudrup
Michael Laudrup akimpa mdogo wake kitambaa cha unaholdha
Michael laudrupp  ni kaka yake na Brian Laudrup ni mmoja kati ya wachezaji bora kukumbukwa katika ardhi ya Denmark akikukumbukwa kwa mafanikio yake aliyopata ndani ya Barcelona Ajax Real Madrid na Juventus. Ni mmoja kati ya viungo waliong’ara kipindi cha Johan Cruyff alipokuwa kocha mkuu wa Barceolna, walipotwaa vikombe tisa ndani ya klabu ya Barcelona. Mwaka 1999 alitajwa kuwa mchezaji bora wa kigeni bora wa ligi kuu Hispania kwa kipindi cha miaka 25. Mwaka 2006 alitajwa na chama cha soka cha nchini humo kuwa mchezaji bora wa Muda wote kutoka Denmark. Wakati Laudrup mkubwa akitajwa kuwa mmoja kati ya wachezaji bora kuwahi kutokea katika nchi za Scandinavia {Sweden, Norway, Denmark n.k} akimpiku mtu kama Zlatan Ibrahmovic pia ni moja kati ya wachezaji waliochezea mahasimu wawili Barcelona Na Madrid na kupata mafanikio katika vipindi vyote. Anatajwa pia kuwa kati ya wachezaji 11 bora kigeni katika historia ya Real Madrid. Kizazi cha akina Laudrup kimeshaondoka Denmark. Kimekuja kizazi kingine kabisa. Kizazi hiki kilianza mizizi yake kwenye michuano ya UEFA ya wachezaji wenye  chini ya miaka 21 mwaka 2014. Kikosi kile kilicheza michuano yote ya kufuzu michuano ile bila kufungwa mchezo hata mmoja kwa kushinda michezo nane na kutoa sare michezo miwili. 
Pierre Emile Hojberg
Pierre Emile Hojbjerg
Katika kikosi kile kilikuwa na kijana mmoja anaitwa Pierre Emile Hojbjerg ambaye akiwa na miaka 14 tayari wanadenmark washamwita Zidane wao. Akiwa na miaka 17 alisajiliwa pale Buyern Munichen. Mwandishi maarufu kwa jina la Jonathan Fadugba mnamo mwaka 2016 alisema kuwa Kijana huyu aliyeanzia maisha kule FC Copenhagen ambaye kwa sasa anakipiga Southampton anaweza akawa na balaa kuliko Staa wa taifa hilo kwa sasa Christian Eriksen anayekipiga Tottenham Hotspur. Kijana huyu akiwa na miaka 17 na siku 251, aliweka rekodi ya mchezaji mdogo kuwahi kucheza kwenye mchezo wa mashindano ndan ya klabu ya Buyern Munichen mnamo mwaka 2013. Mbali na baba yake kukutwa na matatizo ya kansa kocha mkuu wa Buyern bwana Pep Guardiola alimsaidia baba yake na Hojbjerg kuhakikisha anapata matatibu. Hojbjerg anasema siku ya kwanza Pep kukutana na baba yake, Pep alitoa machozi kutokana na hali ile. 

*****************************************************************************
Tukiachana na huyo kuna fundi mwingine aliyemtoa kijasho Jose Mourinho. Anajulikana kama Pione Sisto. Mashabiki wa Man Utd watamkumbuka vyema kwenye mchezo wao dhidi ya Celta Vigo. Ni kiungo wa katikati hivi, mweusi, anakata mbuga kama N’golo Kante vile. Huenda wadernmark wasimsahau Michael Laudrup lakini huyu nae atakuwa moja ya lulu walizobarikiwa kwa miaka ya hivi karibuni ukiachana na Christian Ericksen. Akiwa na miaka 18 alikipiga katika klabu ya Midjylland na alitwaa tuzo ya mchezaji bora wa mwaka akiwa na miaka 18 tu.  Aliifungia klabu ile magoli 20 katika michezo 90, kwa idadi hiyo ya magoli mengi huku akiwa kiungo wa kati tu. Barcelona Juventus Milan na Porto zilimmendea kwa miaka kadhaa kabla ya Arsen wenger nae kupeleka ofa yake. Wakati Man Utd ilipotwangwa na Midjytlland 2-1 yeye alifunga goli moja na alikuwa balaa mbele ya ulinzi wa Man Utd.
Image result for pione sisto
huyu ndiye Mganda Pione Sisto

***********************************************************************************
Pia kuna kijana mwingine anaitwa Andreas Christensen, nadhani mashabiki wa Chelsea wanaweza kumwelezea vizuri maana alijunga na academy ya klabu hiyo akitokea kwenye klabu ya nchini kwao iitwayo Brondby. Cheslea alicheza mchezo mmoja kabla ya kuelekea Ujeruman. Conte alitaka kumrudisha kikosini mwaka huu mwezi wa kwanza. Amekuwa ndiyo kiongozi wa klabu ya Borussia Monchengladbach akiwa na wastani wa 4.5 kati ya 5, akiwa amejikusanyia alama 624 kutokana na kituo maarufu cha kutoa takwimu za wachezaji kijulikanacho kama Squawka. Kwa msimu huu amezuia mipira ya juu kwa asilimia 64, amekuwa na wastani mzuri wa pasi kwa asilimia 90 amemzidi hata Paul Pogba.  Ana uwezo mkubwa wa kuzuia mipira, umakini katika kupiga pasi na utulivu wa kipekee uwanjan, yaani ni kama Michael Laudrupp amerudi tena uwanjani.
***********************************************************************************

Ajax nao wana mdenmark mmoja anajulikana kama Kasper Dolberg ukimwona akiwa amevaa jezi ya Ajax unaweza ukadhani Yule dogo ni mholanzi lakini sio.
Image result for Kasper Dolberg
Kasper Dolberg
Aliyeibua kipaji cha kijana huyu ni Yule Yule skauti aliyewaleta zlatan, Ericken, nad Fischer sokoni. Msimu huu ndani ya Ajax ana magoli 18 na ametengeneza magoli 6 katika michezo 38. Kwa takwimu hizo huyu nae ana balaa nan do kwanza ana miaka 18. Huu ndio kwanza msimu wake wa kwanza kuwa kikosi cha kwanza ndani ya Ajax na tayari ana balaa. Kwenye mchezo wa Mwisho dhidi ya Ajax ndo nilianza kumwelewa huyu kijana baada ya kuipatia klabu yake goli la pili dhidi ya Olympic lyon. Ndani ya Ligi kuu uholanzi tayari ameshafunga magoli 15 latika michezo 25 huku michuano ya ulaya akiwa na magoli 3 kwenye michezo 6 huku michuano ya UEFA akiwa na goli moja katika mchezo 1 tu. Mpaka kufikia sasa yeye ndiye mchezaji bora ndani ya ligi kuu uholanzi akiwa na wastani wa 3.5 [squawka] Nataka pia nikumegee tena na motto mmoja mchafu sana anajulikana kama Jens Odegaard, achana na Martin Odergaad Yule wa Madrid, huyu ana miaka 17 tu, na kwenye michuano ya UEFA ya miaka 17 tayari ameshakuwa gumzo huko. Wadernmark wanamwita Marco Van Bastern wao, ni mshambuliaji wa mwisho. Wapo wachezaji wengi kama kipa wao Peter schmeicel anayekipiga Leicester City, pia yupo Ericksen anayekipiga Tottenham. 
 
Image result for DENMARK BEST FOOTBALL TALENTS
Viktor Fischer
Pia yupo kiungo wa zaman wa Ajax ajulikanae kama Viktor Fischer mwenye miaka 22 ambaye aliichezea Ajax Michezo 80 na kufunga magoli 25 huku akiwa na magoli matatu timu ya taifa kwenye michezo 13 alitajwa kuwa mchezaji chipukizi mara mbili akiwa Denmark na baadae akiwa Ajax, pia akiwa kwenye michuano ya wachezaji wa chini ya miaka 17 aliweza kuifungia timu yake ya taifa magoli 20 katika michezo 30 na waliweza kufika nusu fainali ya kombe hilo kabla ya kufungwa na Ujeruman. Babu yake fischer pia alikuwa mcheza soka wa zaman wa taifa hilo bwana Poul Pedersen ambaye alikuwa akisakata kabumbu kama winga teleza miaka hiyo.
*******************************************
Nini hasa lengo langu kuwazungumzia hawa,? Kwanza ukiangalia taifa la Ubelgiji lilikuja kwenye raman za soka baada ya wachezaji wake wadogo kutambulishwa katika ligi kubwa barani ulaya huku pia wakiwa wachezaji tegemezi ndani ya klabu hizo. Kwa kuangalia namna Ubelgiji walivyovuma, ni kama naoana Denmark wakipitia njia ile ile. Kwa mfano ukiangalia vijana hao wote, wapo chini ya miaka 23, maana yake miaka 6 ijayo Denmark itakuwa na vijana zaid ya 8 ambao tayari ni wachezaji wakubwa na tegemezi katika kikosi chao. Vijana hao wameshaonesha viwango vikubwa kiasi kwamba tayari ni chachu kwa vijana wengine walibakia. Sisto Pione ambaye ni mzaliwa wa Uganda tayari ameshaonesha kiwango cha aina yake. Sisto ameikataa Uganda na kwenda Denmark kwa sababu tayari ameshaona mwanga mbele. Tayari academy za Lyseng IF, academy ya Lyngby BK, Aalborg bila kusahau academy ya Midjytlland ambayo imekuwa gumzo kwasasa. Hizo shule za soka zote tayari zitapata mwamko wa kuzidi kuendelea kuinua vipaji zaid. Natoa angalizo ni mapema sana kufananisha kizazi hiki na kile cha mwaka 1992 kwa upande wa mafanikio lakini tayari wameshaonesha cheche.

Image result for DENMARK BEST FOOTBALL TALENTS
Christian Ericksenn wa Totteham

No comments

Powered by Blogger.