PIIRLO ALITENGENEZA HESHIMA, DONNARUMA HATAKI HESHIMA AMECHOKA KULA DONA





Na Priva ABIUD.
Kijiweni......
Ni miaka 6 imepita tokea mkurugenzi wa zaman wa Ac Milan bwana Adriano Galliani afanye kosa aliloliita kosa lake la maisha. Ni pale alipomruhusu kiungo bora kabisa Andrea Pirlo kujiunga na mahasimu wao wakubwa Juventus.  Kosa alilolifanya Gallian kwa sasa linamtesa mkurugenzi mkuu wa Millan kwa sasa Marco Fassone ambaye ameingia mgogoro mkubwa na Wakala wa Golikipa wa klabu hiyo Gianluigi Donnarumma kwa kila kinachoitwa vita ya pesa.  Donnaruma amedai kuwa anashindwa kuongeza mkataba kwa sababu ametishiwa sana na mashabiki wa klabu hiyo na hata taifa kwa ujumla.
https://tmssl.akamaized.net//images/foto/normal/gianluigi-donnarumma-1478612396-6447.jpg 

 Donnarumma mlinda mlango kwa Ac Milan  kwa sasa anaishi kama mkimbizi ndani ya taifa lake. Hivi majuzi tu kwenye mchezo wa  timu taifa ya vijana ya Italia donnarumma alitupiwa hela feki na mashabiki kwa kile walichodai kuwa bwana mdogo amegomea mshahara wa E80,000 kwa wiki akiwa na miaka 18 tu. Mino Raiola aliyekuwa dalali wa dili la Paul Pogba, ndiye wakala wa Donnarumma, na amekanusha kuwa mteja wake kuwa hajasaini wa sababu za kifedha ila anahofia usalama wake klabuni hapo. Donnaruma alijiunga Ac milan akiwa na miaka 16 akiwa anapata mshahara wa E100,000 kwa mwaka.
Image result for pirlo  ac milan and kissing jerseyAmejipatia umaarufu mkubwa kwa uwezo wake akiwa golini. Mlinda mlango huyu mpaka sasa amecheza michezo 70 tu lakini tayari vurugu la mkataba limekwisha anza.  Kuna baadhi ya mambo ya kuweka sawa, sio kweli kama Donna anataka kuondoka kisa ametishiwa, nani anamtishia? Tangu lini unamtishia mchezaji wako bora kabisa? Raiola kwa sasa ni dalali wakuopogwa kabisa.
 Walio wengi wanamtukana Donnaruma wanasema kuwa anapenda hela kuliko klabu ya Ac Milan.
Kwa akili ya kawaida ni nani hapendi pesa? Yuda Iskarioti mwenywe alimuuza Mwana wa Mungu kisa pesa. Makanisa mengi duniani yanahimiza matoleo ya sadaka, wewe ni nani asiyependa pesa kama viongoz wa dini wanatuhubiria kuhusu sadaka? Hivi unajua kazi anayoifanya Donnaruma pale golini? Yaani mtu anajitupa kufuata mashuti ya watu mnasema anapenda hela? Mlitaka apende nini?Cha muhimu katika maisha ya mchezaji kwanza ni maslahi yake. Huwezi kutegemea kazi ya mchezaji bila kutimiza maslahi yake. Wapo watu wanaodai kuwa wachezaji wa siku hizi wanataka fedha nyingi ukilinganisha na wa zamani.Naamini watu watakuja na mfano wa Messi kugomea waraabu wa Man city na PSG kuwa hapendi hela. Kuna tofauti kubwa sana hapa, fahamu kuwa kuna tofauti ya mchezaji aliyeridhika na pesa anazopata na yule ambaye yeye anaona alizo nazo bado ni kidogo.Mshahara wa Messi pamoja na mafanikio yake yanamtosha
Image result for Patrick William "Willie" Groves
Willie Groves
kabisa kususia fedha za klabu ambazo haziwezi kumpa mafanikio hayo. Donnarumma yupo kwenye timu ambayo haina mbele wala nyuma kwa sasa na bado mshahara ni mdogo je aendelee kubaki kisa anaogopa ataambiawa anapenda fedha nyingi? Hivi fedha nyingi ndo nini? Kipi ni kipimo cha fedha nyingi? Dunia imebadilika sana. Ulitegemea mchezaji ambaye ana kipaji kizuri apatikane kwa ada ya million 20? Kwani tupo mwaka 2000? Hivi hao wazungu wanaotoa hizo fedha kwan wao hawaoni kama ni nyingi? Ni kweli kiasi ambacho Moratta anahitajika nacho Man Utd ni nyingi sawa, ila ni nyingi kwa wakati gani? Ngoja leo niongee kiuchumi kidogo ili kidogo nieleweke, kwanza nataka nikwambie kila baada ya miaka 7 mpaka 10 kuna uwezekano mkubwa  thamani ya kitu ikawa mara mbili zaidi ya kilivyo kuwa kiuchumi. Usiniulize ni nani kasema, nimesema mimi mwenyewe. Nikukumbushe tu, mwaka 2000 dola 1 ya Marekani ilikuwa sawa na shilingi 800 ya Tanzania, leo hii dola 1 ni sawa na 2300, hii inaashiria nini? Uchumi umebadilika sana. Nikurudishe mbali sana,  mchezaji wa kwanza kabisa duniani kuuzwa alikuwa Willie Grove aliuzwa E100 kutokea West Bromwich albion na kwenda Aston Villa mwaka 1893, ilipita takribani miaka 12 ile rekodi kuvunjwa na mchezaji aliyefuata aliuzwa takribani E1000 ambapo mshambuliaji hatari wa Sunderland kwa wakati ule Bwana Alf Common alipouzwa kwa Middlesbrough. Ukiangaliahiyo bei ni sawa na takribani mara 10 ya bei ya hapo awali.
Hivi hata nyie mashabiki wa Arsenal mnaosema Arsene Wenger ni mbahili hamjui kuwa kocha wenu wa zaman Bwana Herbert Chapman aliweka rekodi ya kumnunua mchezaji wa gharama kubwa mwaka 1928, walitoa kitita cha E10,000 ili kumpata David Jack kutoka Bolton Wanderers hapo ilikuwa takriban miaka 10 baadae.


Image result for David Bone Nightingale Jack
katikati Bwana David Jack

 Nadhani mpaka hapo unaelewa nini nachomaanisha. Bei za wachezaji zinapanda kutokana na hali halisi ya uchumi kwa wakati huo. Au nikupe mfano rahisi tu, mwaka 2008 gari la kifahari aina ya Buggati Veyron 16.4  liliuzwa dola million 1 na ushee, lakini gari lile lile kwa mwaka 2015 linauzwa takribani dola milion 2.5, hii ni mara mbili ya bei ya hapo awali. Maisha yanabadilika, uchumi unapanda, bei ya maisha inaongezeka kwa kiasi kikubwa. Bei ya Pirlo akiwa na miaka 22 ilikuwa E18 mnamo mwaka 2001, lakini huwezi kumpata kiungo mkabaji mzuri kama Pirlo kwa wakati kwa bei hiyo hata kidogo.
Image result for pirlo  ac milan and kissing jersey N’golo Kante tu ameigharimu bei kubwa sana chelsea ukilinganisha na bei ya Pirlo ambayo ni mara mbili. Nawashangaa sana Mashabiki wa Ac Milan ambao  wamepoteza muda wao wakizunguka mitaa ya Santa Maria Dele gracie kwenye steshenari za Fabriano Boutique, Pettinaroli na na wengine wakijazana maduka ya San Maurilio na Pasini Milano kuprint hela bandia ili wakamtupie Donnoruma kile wanachodai anataka pesa nyingi. Nimesema hapo awali kuwa bei ya maisha inabadilika mara mbili zaid ya hapo awali kwa takribani miaka 5 na kuendelea. Niwarudishe nyuma kidogo wala sio mbali sana, najua unamfahamu Zinedine Zidane? Mwaka 2001 si unafaham alikuwa Juventus? bila shaka ni ndio. Unafahamu kuwa mwaka ule ule alihamia Real Madrid? Je unafahamu alisafirishwa kwa kitita cha E46? Jibu ni ndio namba hazidanganyi. Je unafahamu ilichukua miaka mingapi kwa bei ile kuzidishwa mara mbili kwenye usajili mwingine? Ilichukua miaka 7 tu, ambapo Cristiano Ronaldo alipatikana kwa ada ya E80. Je ulitaka Ronaldo nae auzwe sawa na bei ya Zidane aliyeuzwa miaka ya 2001 kisa tu pesa hiyo ndo sahihi na sio nyingi?



Image result for most expensive transfer 
Nmeuliza tokea awali pesa nyingi ndo nini? Kipi ndio kiwango cha pesa nyingi? Je tutumie kigezo gani kusema pesa ni nyingi? Twende taratibu tu utanielewa. Najua unamfaham Juan Veron? Bila shaka unamfahamu. Huyu aliweka rekodi ya kununuliwa ghali zaid mwaka 2000 kiasi cha E28, katika ligi kuu ya England alipojiunga na Man Utd. Je unafahamu ilichukua muda gani ili mchezaji apatikane kwa mara mbili zaid ya bei ile? Naam mwaka 2014 Angel Di maria aliweka rekodi hiyo kwa kitita cha E58 akijiunga Man Utd ile ile iliyoweka rekodi ya awali. Nataka niwaambie kitu ndugu zangu, nadhani ni vyema bei zikalinganishwa kwa miaka ili kupata uwiano mzuri na sio tu kisa namba zikionekana nyingi basi hiyo pesa n nyingi sana. Mfano mwingine  mrahisi,  tujikumbushe hapo awali, miaka ya 2000 soda tulinunua shilingi ngapi? Sio 200 kweli? Je leo hii 200 unapata nini? Je miaka ya nyuma unakumbuka thaman ya senti tano? Je bei ya soda kwa sasa na kwa wakati ule sio mara mbili?

Kwanini tunawalaumu akina Mbappe wakitakwa kwa E130? Unadhani wazungu wamewehuka? Maisha yamebadilika mno. Thamani ya pesa inapanda sana. Unategemea Donnarumma hapendi maisha mazuri? Hivi ni kweli kwamba hapendi kutembelea  gari ya lakshari kama Buggati Veryon? Unadhani yeye hapendi kupumzika hoteli za kifahari kama  Pallazo Parigi kule milano? tena kwenye vyumba vya gharama kabisa? Unafikiri hapendi kwenda fukwe za Puglia na San Vitolo Capo kule sicily kula bata wakati wa mapumziko na familia yake? Yaani kwa akili yao wanafikiri Donnarumma anapopigiwa mashuti golini na kudaka kama mtu asiye na akili kwamba hawazi maisha mazuri?
Twendeni mbele turudi nyuma, ukisikia E100 usidhani kwa wenzetu ni nyingi sana kama tunavyowaza hapa kwetu bongo. Ukweli ni kwamba klabu kama Man Utd na Madrdi zina takribani utajiri wa Dola billion 3 na ushee kila moja. Sasa kama timu ina utajiri huo kumnunua mchezaji ghali sie kinatuuma nini? Yaani leo hii Bakhresa amenunua andazi la 100 kwa 1000 unalalamika?
Mimi sioni kama ni matumizi mabaya ya fedha nachokiona ni mabadiliko yametokea kwenye uchumi wa dunia. Siku hizi wametokea mawakala virambasi sana, na wenyewe wanataka cha juu kwenye kila dilia wanalo piga, je unategemea utampata mchezaji kwa bei za mbuzi? Huna pesa kaa kimya. Usiseme kama Man Utd inaharibu soka kwa kununua wachezaji ghali kwamba timu ndogo zitashindwa kufanya usajili, kwani timu gani ndogo imenunua mchezaji ghali? Kama hazijawahi shida iko wapi Man Utd na liverpool zikimwaga hela? Msinielewe vibaya, hapa sizungumzii soka la biashara la wachina. Wale wanajielewa wao wenyewe, nao wana mipango yao. Hao si wazungumzii kabisa.Related image

Kiuhalisia milion 100 kwa sasa ni sawa na Million 40 ya miaka 10 iliyopita wala hilo halipingiki kabisa. Labda tu nikukumbushe rekodi zilitolewa na Delloite kuhusu mapato ya Real Madrid na Man Utd kwa kipindi cha kuanzia mwaka 2001 hadi 2011, mwaka 2001 zote kwa pamoja ziliikusanyia zaid ya million 350, lakini kufikia mwaka 2011 zote zilijikusanyia mapato ya takribani million 800, sasa unategema nini? Kama timu inapata mafanikio makubwa kiasi hiki kama tunavyoona kwanini wachezaji nao bei zao zisipande? Sasa kama Ac Millan imenunuliwa kwa mkataba wa zaid ya billion 1, lakini bado Donnarumma analipwa 100, 000 kwa mwaka unategemea nini? Kwanza Donnarumma anataka zaid ya million 10 kwa mwaka. Ashafahamu kuwa ana kipaji ambacho kinauzika kwa gharama yoyote kwa sasa duniani. Sasa ya nini masikini kumpangia tajiri namna ya kutumia hela? Umri wa mchezaji sio tatizo kabisa, kwani Henry alinunuliwa bei gani na alikuwa na Umri gani? Je kuna mtu alitegemea balaa la henry hapo baadae? Maana henry alinunuliwa E16 akitokea Juve akiwa na miaka 20 tu, lakini  kila mtu alimnyooshea kidole Wenger. Lakini Rekodi ya Henry inakuja kuvunjwa baada ya miaka 13 na Mesut Ozil aliponunuliwa kwa ada ya E47 akiwa na miaka 24. Je ulitegemea kumpata ozil kwa bei ya Henry ya mwaka 2000 kweli? Labda nikuulize swali la kizushi tu, si unafahama Coutinho wa liverpool? alinunuliwa Million 7 akitoke Inter mwaka 2013? Je ingekuwa ndio sasa hivi yupo Inter angeuzwa bei hiyo hiyo kweli? Narudia tena heshima zipo jeshini kwenye soka cha kwanza maslahi. Siku njema.

No comments

Powered by Blogger.