RANIERI NENDA SOFAPAKA, KISHA RUDI KING STREE NA QUEEN STREE UANGALIE ILE SANAMU



RANIERI NENDA SOFAPAKA, KISHA RUDI KING STREE NA QUEEN STREE UANGALIE ILE SANAMU


MIWANI YANGU.
Mnamo mwaka 2009 sofa paka walitwaa ubingwa wa KPL yaan ligi kuu ya Kenya. Hakuna aliyedhani klabu ndogo kama ile ingeweza kufurukuta mbele ya timu kama Gor mahia, tusker na klabu nyingine kubwa Kenya kama FC leopard kama wanavyojiita wenyewe INGWE. Mwaka uliopita pale England nako palitokea maajabu kama haya haya ya Kenya Leicester city anatwaa ubingwa mbele ya timu kubwa nne za England. Msimu wa England umeanza tena, kila mtu ana neno lake la kuongea, wakati EPL inaanza Kenya jadithi nayo ni tofauti kidogo, wale mabingwa wa 2009 sofapaka wanapambana na Ushuru FC pamoja na Nairobi city star kutokusuka daraja. Sofa paka kwa sasa wamejikusanyia alama 15 tu huku nairob city ambao wao wana alama 14. Ushuru fc wao tayari wameweka kibindoni alama 22 huku wote wakiwa wamecheza michezo 23. Nairobi city star wao wanashikilia mkia wakiwa wako nafasi ya 15, sofa paka 14 kisha ushuru 13. Wote hao wanapambana kutokushuka daraja. Anaeongoza ligi kwa sasa ni tusker FC ikiwa na alama 44 huku wakifuatwa kwa karibu sana na Gor mahia wakiwa na alama 37 na mchezo mmoja mkononi. 

Image result for SOFAPAKA 

Mlinzi wa zamani wa Mathare United Noah abich ambaye kwa sasa anakipiga sofapaka juzi nilimnukuu maneno yake akisema kuwa ni ngumu kwa sofa paka kushuka daraja, watapambana mpaka jasho lao la mwisho kuhakikisha kuwa wanabaki ligi kuu nchi Kenya. Sofa paka ambao wanajulikana kama Batoto Ba Mungu msimu huu walikumbwa na matatizo lukuki ya kifedha yaliyopelekea klabu hii kupoteza takribani wachezaji 21 ingawa ilisajili wachezaji wapya 25 ambao wote walikuwa wakiwango cha kawaida. Klabu ya sofapaka ilipoteza wachezaji wake wa kikosi cha kwanza wote. Mchezaji wao hatari John Barry ama kwa jina lake kamili John baraza alistaafu kucheza soka na akaamua kujiunga na benchi la ufundi la klabu hiyo. Mnamo mwezi wa kwanza Mwenyekiti wa klabu hiyo Bwana Elly Kalekwa alipitia katika wakati mgumu kifedha kitu ambacho kilimfanya kocha mkuu wa klabu hiyo David Ouma kutangaza kuwa klabu hiyo haina uwezo wa kuwanunua wachezaji wenye majina makubwa.

Image result for john barasa
John barasa akiwa na tuzo ya mchezaji bora mwaka 2010
Tukirudi Pale England Jamie Vardy ana miaka 29, muda sio mrefu nae ataanza pensheni hasa kutokana na mfumo wa ligi kuu, Leicester city tayari wameshampoteza mchezaji wao mahiri kabisa N’golo kante, amekuja Mussa ambaye binafsi yangu namwona ni mwoga sana, bado ana roho ya kiafrika ya kuogopa kukosea mbele ya rangi nyeupe, bwana mdogo grey bado ni mzito nae ana akili inayoendana na rangi yake mzito kufikiri na kutoa maamuz ya haraka. Leicester city uliyoanzishwa miaka 132 iliyopita wanarudi EPL tena sijajua wanatetea ubingwa au wanapambana na hali yao. Tukirudi takribani miaka 40 hivi, Nottingham forest walipanda ligi kuu England mwaka 1978 na wakatwaa ubingwa sawa tu na sofapaka na Leicester city. Msimu uliofuata Nottingham walimaliza ligi wakiwa chini ya Liverpool kwa alama 60 liverpool wakiwa na alama 68 huku mshambuliaji hatari wa kiingireza Garry Birtles akifunga magoli 14 na kuwa mfungaji bora wa klabu hiyo. Kwa upande wa pili huku Kenya msimu wa pili wa sofa paka wao walitwaa kombe la shirikisho huku ulinzi stars wakitwaa ubingwa, walishinda pia kombe la Rais. John baraza aliibuka kidedea kama mfungaji bora kwa jumla ya goli 15.


Image result for jamie vardy award
jarmie vardy akiwa na tuzo ya mchezaji bora wa mwezi msimu wa 2015
Image result for trevor francis
trevor francis akiwa na kombe la UEFA 1979
Leicester wana kazi nzito msimu huu, Jarmie Vardy alivunja rekodi ya Ruud Van Nestelrooy kwa kufunga magoli 13 kwenye michezo 11. Msimu huu wameuza ghali na wamenunua ghali, kante ameondoka kwa Ada ya E30 na wamemnunua Islam Sliman kutoka sporting CP kwa ada ya E29 ikiwa ni rekodi kwa klabu hiyo. Nottingham nao msimu wa 1978 hawakuwa nyuma kwenye usajili Ingawa walisajili wachezaji wawili tu, Garry milly aliyetokea klabu ya watoto na Trevor fransic aliyetokea Birmingham city kwa ada ta 1,000,000 aliyweka rekodi ya usajil, lakini walimuuza Peter white kwa ada ya 200,000 kwenye Newcastle. Msimu huo wa 1979 nottingham forest ikiwa ni kwa mara yao ya kwanza kushiriki kombe la Yuropa ambalo kwa sasa ni UEFA ilitwaa ubingwa ule. Narudia tena. Msimu huo wa 1979 nottingham forest ikiwa ni kwa mara yao ya kwanza kushiriki kombe la Yuropa ambalo kwa sasa ni UEFA ilitwaa ubingwa ule. Mwaka huo huo walitwaa charity shield, na kombe la ligi ambao wengi wanaliita Carling Cup kwa sasa likijulikana kama fly emirates Fa cup. Fainali ya YUropa walicheza na malmo Fc na Francis aliwainua waingereza kidedea katika ardhi ya Ujeruman kwenye uwanja wa Olympiastadion ulikuwa ukibeba takriban ya mashabiki 57,000.


Sofapaka na Nottingham wanaonekana kutoa somo kwa Leicester city. Ranieri hapaswi tu kuangalia Man united wamemsajili pogba kwa gharama kubwa, gharama kubwa waati Fulani sio tija. Itakuwa aibu kubwa sana kama tutaona Leicester wanapambana kutokushuka daraja. Nottingham wao msimu wa pili hawakuhangaika kushuka daraja, ule msimu Chelsea na Birmingham wao ndo walioshuka daraja. Tusitegemee vipigo vya haja kwao maana ule msimu tottenham ndiye aliyepewa visago vya maana Liverpool 7 0 tottenham, tottenham 0 5 arsenal. Nadhani ni wakati wa Leicester city kuonesha kuwa wao hawajabahatisha. Imechukua takriban miaka 7 ndipo sofapaka anaelekea kushuka daraja. 


Brian Clough alikuwa kocha wa Nottingham kwa miaka takriban 18 na ndiye kocha mwenye mafanikio makubwa zaid ndani ya klabu hii,
Image result for brian clough 
Brian Clough ametengenezewa sanamu kubwa maeneo ya King street kwa mafanikio makubwa aliyoyapata, je ranieri anaweza kuwekewa sanamu ndani ya nchi ya watu? Kwa lipi? Labda Leicester city wakutengeneze, ila je utatengenezewa sana kwa heshima kama ya Clough? Kama ranieri anahitaji heshima ya clough kwanza inambidi afanye makubwa ambayo waingereza watamthamin.



Huenda Ranieri nae akaonekana kocha mwenye mafanikio ya kipekee, lakini Ranier atathaminika kama clough endapo tu atafanya mambo makubwa msimu huu. Yaani asitoke kapa kabisa. Nottingham walitwaa tena kombe la UEFA mwaka uliofuata. Je Leicester nao watwae uefa? Daah ni kama nawaonea Leicester city hasa katika kizazi hiki cha Messi na Ronaldo.


Labda tuipe Leicester city mtihani mrahisi tu, msimu huu wapambane kubaki nafasi tano za juu, au afike hatua ya robo fainali ya UEFA kama huko kugumu basi tumwone Uropa akifika nusu fainali. Vipi huu mtihani utamfaa Ranieri? Kama Ranieri hakubahatisha basi afanye hayo maswali niliyompa hapo juu. Vipi bado ni mgumu?
Image result for claudio ranieri with uefa
claudio ranieri akiwa na ubingwa wa ligi
Mtihani wa clough ulikuwa mgumu sana. Yaani timu imepanda daraja na inachukua ubingwa wa ligi na kutwaa UEFA kwa miaka miwili mfululizo? Sasa ugumu wa Ranieri uko wapi? unadhani miaka ile hakukuwa na mafundi? 

Image result for brian clough
brian Clough akiwa na kombe la UEFA

Walikuwepo akina Bryan Robson aliyenunuliwa million 1.7 na Manchester united mwaka 1980. Hawa Nottingham wenyewe walikuwa tayari kutoa Million 1 ikiwa na mchezaji wa kwanza kutoka England kununuliwa ghali mno, je Leicester mmesajili nani? Je mtashinda huu mtihani kweli? Kuna mwanaume mwingine alielekea wolverhampton akitokea  aston villa kwa million 1.4 bwana andy grey. Kuna mwingereza mmoja alikuwa fundi sana kevin Keegan miaka ile alikua hamburg, kuna kijana mwingine alikuwa hatari sana kwa kunyumbulika wazee wazamani walivyokuwa wanamwita ndugu Laurie cunnigham alipokuwa pale Madrid, aisee huku werder Bremen wazee wa vunja vunja alikuwepo bwana David Watson, sasa tukienda ufundini walikuwepo akina zico, Socrates, edinho, na mwanaume falcao. Sio kwamba hakukuwa na mastaa kama sasa, walikuwepo. Ranieri nenda Kenya ukishagundua kwanini sofa paka waanazingua Rudi sasa mpaka West Bridgford kisham mtafute fawaz Al hasawi mwombe ruhusa ya kuongea na bwana Philippe Montainier, mwambie Montanier kuwa umeongea na bosi wake ustazi hasawi akakuruhusu uongee nae ili akuoneshe makabrasha aliyoacha huyo kocha wa zamani wa Nottingham brian Clough ili ujue alifanikiwa vipi miaka ile ya 70 Plz ranieri no excus do the exams. Wish you luck.
Nottingham Forest, under Brian Clough, shocked the football world by winning the First Division in 1978
clough alikuwa anapigisha pindi hata wakiwa safarini

No comments

Powered by Blogger.